1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wito wa vita kusitishwa Gaza kupisha chanjo ya polio

29 Agosti 2024

Nchi 27 wanachama wa Umoja wa Ulaya wametoa wito kwa Israel na Hamas kusitisha vita Gaza kwa sababu za kiutu, ili kuruhusu kuanza kwa kampeni ya chanjo ya polio.

https://p.dw.com/p/4k3oC
Gazastreifen El-Zawaida | Polio-Impfungen in Gaza
Picha: Omar Ashtawy/APA Images/Zumapress/picture alliance

Umoja huo umeungana na miito iliyotolewa na Umoja wa Mataifa na Shirika la Afya Duniani, WHO, la usitishwaji wa mapigano ili kuruhusu maafisa wa afya kuwapa chanjo watoto.

Umoja wa Ulaya pia umepongeza utoaji wa zaidi ya dozi milioni 1.2 za chanjo za polio, pamoja na ushirikiano wa Israel katika kuzipeleka chanjo hizo Gaza.

Wakati huo huo, kiongozi wa upinzani wa Israel, Yair Lapid amekataa madai yaliyotolewa na Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwamba kiongozi wa Israel hakupokea onyo kuhusu shambulizi la Hamas.

Lapid ameliambia gazeti la Jerusalem Post kuwa Netanyahu alipewa taarifa, na yeye mwenyewe aliarifiwa, na taarifa hiyo ilitolewa kwa baraza la mawaziri.