Watu 27 wameuawa katika shambulizi Burkina Faso
11 Machi 2024Matangazo
Duru zinaeleza kwamba mkasa ulitokea Ijumaa iliyopita wakati wakazi wakiwa wamekusanyika kusherehekea Siku ya Wanawake ya Kimataifa.
Wakati wa shambulio hilo, kiongozi wa muda Ibrahim Traoré, ambaye anaongoza serikali ya kijeshi, alikuwa anawatembelea wanajeshi katika miji ya karibu ya Tenkodogo na Bagré.
Makadirio yanaonesha kuwa serikali inadhibiti karibu nusu tu, ya eneo hilo la taifa la Afrika Magharibi lenye watu milioni 23.