1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON: HEROIN YAHATARISHA UTULIVU

5 Machi 2005
https://p.dw.com/p/CFZX

Kwa mujibu wa ripoti ya wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani,mazao ya heroin nchini Afghanistan ni kitisho kikubwa kwa utulivu duniani.Ripoti hiyo iliyotolewa siku ya Ijumaa inaonya kuwa Afghanistan inakaribia kuwa taifa la madawa ya kulevya.Vile vile ripoti inaonyesha kuwa eneo linalotumiwa kupanda mipopi nchini Afghanistan limeongezeka kwa mara tatu katika muda wa miaka miwili.