1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanajeshi wa Djibouti wamewasili Somalia

Martin,Prema/afpe21 Desemba 2011

Kikosi cha kwanza cha wanajeshi 100 kutoka Djibouti kimewasili Mogadishu jana kuungana na vikosi vya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) vinavyopigana na makundi ya al-Shabaab yenye mahusiano na al-Qaeda.

https://p.dw.com/p/13WpZ
African union peacekeepers in Somalia patrol in a tank as they assists government forces during clashes with Islamist insurgents in southern Mogadishu, Somalia, on Monday Aug. 16, 2010. (AP Photo/Farah Abdi Warsameh)
Vikosi vya Umoja wa Afrika vinasaidia kulinda usalama SomaliaPicha: AP

Wanajeshi wengine 800 watawasili wiki ijayo au baadae. Wanajeshi hao wa Djibouti wanaozungumza Kisomali, watashirikiana na wanajeshi 9,800 kutoka Burundi na Uganda waliopo Somalia tangu mwaka 2007 kuilinda serikali ya Somalia katika mji mkuu Mogadishu.
Brigedia-Jenerali Audace Nduwumunsi wa vikosi vya Umoja wa Afrika nchini Somalia amesema, kuwasili kwa kikosi hicho cha Djibouti ni hatua kubwa kwa AMISOM na jitahada za kuleta utulivu nchini Somalia.