1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waliokufa kwa kuacha kula Kenya wapindukia watu 300

14 Juni 2023

Idadi ya waliofariki katika uchunguzi unaohusishwa na dhehebu la kidini huko Kenya ambalo wafuasi wake waliishi bila ya kula kwa imani ya kukutana na Yesu Kristo imepindukia 300 baada ya miili 19 zaidi kupatikana.

https://p.dw.com/p/4SXog
Kenyans seek relatives among starvation cult victims in Malindi
Picha: Monicah Mwangi/REUTERS

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Rhoda Onyancha alisema idadi ya waliofariki hadi wakati huu  imeongezeka na kufikia watu 303 baada ya miili 19 kufukuliwa.

Polisi ya inaamini kuwa miili mingi iliyopatikana katika msitu karibu na mji wa Malindi katika Bahari ya Hindi ni ya wafuasi wa Paul Nthenge Mackenzie, dereva wa teksi ambaye amegeuka kuwa mhubiri ambaye amekuwa chini ya ulinzi wa polisi tangu Aprili 14.

Soma pia: Kenya kuugeuza msitu wa Shakahola kuwa kituo cha kumbukumbu

Mtuhumiwa huyo anatarajiwa kukabiliwa na mashtaka ya "ugaidi" katika kesi ambayo imetikisa taifa hilo la Afrika mashariki.