1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wagombea wote wadai ushindi Madagascar

Sekione Kitojo
20 Desemba 2018

Wagombea wote katika uchaguzi wa duru ya pili nchini Madagascar wamedai ushindi baada ya uchaguzi huo.

https://p.dw.com/p/3AQm1
Madagaskar, Antananarivo: Wahlen des Präsidenten
Picha: picture-alliance/AP/K. Dhanji

Wagombea  wote  katika  uchaguzi  wa  duru  ya  pili nchini  Madagascar  wamedai  ushindi  baada  ya  uchaguzi huo  uliofanyika  jana, licha  ya  kuwa  ni  asilimia  ndogo ya  matokeo  iliyokwisha  tolewa.

Maraisa  wawili  wa  zamani  walioshiriki  katika  uchaguzi wa  jana  Jumatano  wa  duru  ya  pili  Marc Ravolomanana na  mtu  ambaye  alimuondoa  madarakani  mwaka  2009 katika  mapinduzi, Andry Rajoelina, na  taifa  hilo wanamatumaini  ya  matokeo  ya  amani  na  kuturejewa machafuko  ya  kisiasa  ya  karibu  muongo  mmoja uliopita.

Tume  ya  uchaguzi  ya  Madagascar  imesema  matokeo kutoka  asilimia  5  ya  vituo  vya  uchaguzi  yanaonesha Rajoelina , ambaye  namba  yake  ya  kugombea   katika orodha  ya  wapiga  kura  ni  13, akiongoza  kwa  asilimia 57.