1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani: Wagombea Ukansela wachuana kwenye mdahalo

17 Februari 2025

Wanasiasa wanne wa Ujerumani wanaowania nafasi ya Ukansela walishiriki siku ya Jumapili kwenye mdahalo wa moja kwa moja kwenye televisheni.

https://p.dw.com/p/4qZPu
Olaf Scholz, Robert Habeck, Friedrich Merz na Alice Weidel kwenye mdahalo
Wanasiasa wanne wa Ujerumani wanaogombea Ukansela: kuanzia kushoto: Olaf Scholz, Robert Habeck, Friedrich Merz na Alice Weidel wakishiriki mdahalo.Picha: Kay Nietfeld/dpa-Pool/picture alliance

Wagombea hao walijadili mada muhimu kuhusu Ujerumani na masuala ya kimataifa.

Olaf Scholz, Friedrich Merz, Robert Habeck na Alice Weidel, walishindana kwa hoja kuhusu sera ya uhamiaji, vita vya Ukraine na mdororo wa uchumi ikiwa imesalia karibu wiki moja tu kabla ya uchaguzi mkuu wa kitaifa.

Kansela wa sasa wa Ujerumani Olaf Scholz aliitetea rekodi ya utawala wake kufuatia ukosoaji wa mpinzani wake wa kihafidhina Friedrich Merz, ambaye kura za maoni zinaupa kipaumbele muungano wa chama chake cha CDU na CSUkwa asilimia 30.

Licha ya majibizano makali, kulishuhudiwa pia katika mdahalo huo kauli zinazoashiria umoja kati ya Scholz, Merz na Habeck hasa katika suala la kuendeleza msaada kwa Ukraine na kukosoa kauli za viongozi wa Marekani kuhusu demokrasia ya Ulaya na mazungumzo yajayo ya amani katika mzozo wa Ukraine.