1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yashutumiwa kashambulia hospitali Ukraine

10 Julai 2024

Mashambulizi makali ya anga ya Urusi nchini Ukraine, ikiwa ni pamoja na shambulio la bomu lililoharibu hospitali ya watoto mjini Kiev, yameibua shutuma kali kimataifa katika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la UN

https://p.dw.com/p/4i6IC
Vita vya Ukraine | Baada ya shambulio la Urusi kwenye hospitali ya watoto ya Okhmatdyt
Baada ya shambulio la Urusi kwenye hospitali ya watoto ya Okhmatdyt - Wafanyakazi wa uokoaji wakiondoa vifusi katika hospitali ya watoto ya Okhmatdyt iliyopigwa na makombora ya Urusi Jumatatu, huko Kyiv, Ukraine, Julai 9, 2024. Picha: Evgeniy Maloletka/AP Photo/picture alliance

Wakati wa mkutano huo, afisa mmoja wa Umoja huo, alilaani shambulio hilo na kulitaja kama uhalifu wa kivita huku wafuasi wa Ukraine kwa mara nyingine tena wakishtumu uvamizi wa Urusi nchini humo. Mwakilishi wa Ufaransa, Nicolas de Rivière, aliutaja uvamizi huo wa Urusi kuwa suala jipya katika orodha ya uhalifu wa kivita ambapo Urusi inapaswa kuwajibishwa. China, mshirika wa Urusi, pia ilionyesha wasiwasi katika matamshi ambayo yanaweza kuonekana kama ishara kwa Moscow. Naibu balozi wa China katika Umoja wa Mataifa Geng Shuang, amesema kwa bahati mbaya, mapigano nchini Ukraine yameongezeka na mara kwa mara kumekuwa na mashambulizi ya kikatili ambayo yamesababisha mauaji ya watu wengi. Hata hivyo China imedumisha uangalifu wake wa kawaida na haikumshtumu moja kwa moja mshirika wake wa karibu Urusi.