Urusi yakataa pendekezo la kubadilishana maeneo na Ukraine
12 Februari 2025Msemaji wa Ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov amewaambia waandishi wa habari kwamba Urusi haijawahi na kamwe haitafanya majadiliano kuhusiana na kubadilishana maeneo na Ukraine.
"Dmitry Peskov: Hili haliwezekani. Urusi hijawahi kujadiliana na kamwe haitajadiliana na Ukraine suala hili la kubadilishana maeneo. Na, kwa hakika vikosi vya Ukraine vitafukuzwa kwenye maeneo hayo. Kila mmoja ambaye hataangamizwa, atafukuzwa."
Soma pia:Zelensky: Ukraine iko tayari kubadilishana eneo la ardhi na Urusi
Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine aliyetoa hoja hiyo amesema mashambulizi haya ya karibuni yanaonyesha Urusi haiko tayari kwa mazungumzo ya amani na Ukraine.
Ameandika kwenye mtandao wa X kwamba Rais Vladimir Putin hayuko tayari kwa amani, kwa kuwa anaendelea kuwaua Waukraine na kuharibu miji.