1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tinubu aahidi kushughulikia madai ya raia

5 Agosti 2024

Rais wa Nigeria Bola Tinubu ametoa wito wa kusitisha maandamano makubwa ya kupinga ongezeko la gharama za maisha nchini humo.

https://p.dw.com/p/4j7PZ
Nigeria Maandamano
Raia nchini Nigeria wanapinga kupanda kwa gharama ya maisha.Picha: Sunday Alamba/AP/picture alliance

Kiongozi huyo wa Nigeria amesema mikutano ya kampeni imegeuka na kuwa ya vurugu akiwalaumu watu wachache wenye ajenda ya kisiasa kwamba ndio wanaochochea maandamano hayo.

Licha ya wito huo, maandamano hayo bado yanaendelea katika maeneo machache, ikiwa ni pamoja na mji wa Lagos ambao ni kitovu cha uchumi nchini Nigeria.

Soma zaidi: Watu 13 wauawa katika siku ya kwanza ya maandamano Nigeria

Rais Tinubu katika hotuba yake ya kwanza kwa umma juu ya maandamano hayo amesema anaelewa machungu na mfadhaiko uliosababisha watu kandamana, lakini amewahakikishia Wanaigeria kwamba serikali yake imejitolea kusikiliza na kushughulikia wasiwasi wa wananchi. 

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeripoti vifo vya waandamanaji tisa katika makabiliano na polisi, na watu wengine wanne waliouawa kwa bomu. Hata hivyo, polisi wa Nigeria wameikanusha ripoti hiyo ya Amnesty International.