Mihadarati na matumizi yake ni suala ambalo limesalia kuwa tatizo kubwa katika jamii. Visiwa vya Zanzibar havijasazwa vikiwa na zaidi ya vijana 10,000 ambao ni watumiaji. Katika makala ya Vijana Tugutuke, Salma Said anaangazia jinamizi hilo hasa dawa mbadala aina ya methanol kwa vijana wanaojaribu kuachana na mihadarati.