1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shughuli ya kuhesabu kura imeanza nchini Nigeria.

19 Machi 2023

Shughuli ya kuhesabu kura imeanza nchini Nigeria baada ya kufanyika uchaguzi wa kuwachagua wabunge.

https://p.dw.com/p/4Otlz
Nigeria | Auszählung Wahlen
Picha: Sunday Alamba/AP Photo/picture alliance

Shughuli ya kuhesabu kura imeanza nchini Nigeria baada ya kufanyika uchaguzi wa kuwachagua wabunge. Uchaguzi huo umefanyika wiki tatu baada ya chama tawala nchini humo kushinda uchaguzi wa urais ambao unapingwa na upinzani unaodai kuwa uchaguzi huo uligubikwa na udanganyifu. Nigeria, taifa lenye watu wengi zaidi barani Afrika linawachagua zaidi ya wabunge 900 wa mabunge ya majimbo pamoja na magavana 28, kwenye uchaguzi uliokuwa na ushindani mkubwa hasa katika mji mkuu wa kibiashara wa Lagos.