1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Shinikizo laongezeka kwa May kujiuzulu

Sekione Kitojo
23 Mei 2019

Waziri mkuu wa  Uingereza  Theresa May yumo katika  shinikizo kubwa  kutaja tarehe ambayo ataondoka  madarakani baada  ya juhudi zake za mwisho za mpango wa kujitoa  kutoka  Umoja  wa Ulaya, yaani  Brexit kushindwa,

https://p.dw.com/p/3IwP5
Belgien Brexit-Gipfel in Brüssel
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa MayPicha: Reuters/Y. Herman

Hali hiyo inaondoa mtazamo kutoka uchaguzi wa Ulaya  ambao  hali itaonesha kwamba Uingereza bado inakabiliwa na mgawanyiko kuhusiana na suala  la talaka kuachana na Umoja wa Ulaya. 

Wakati  kuna  mkwamo mjini  London, taifa  hilo lenye  uchumi mkubwa  wa  tano  duniani  linakabiliwa  na tafakuri  nyingi , ikiwa  ni pamoja  na  kujitoa  kwa  utaratibu  mzuri  kwa kupata makubaliano, kujitoa  bila  makubaliano, uchaguzi  ama  kura ya  pili  ya  maoni.

Großbritannien Theresa May, Premierministerin vor Dowing Street 10 in London
Theresa May waziri mkuu wa UingerezaPicha: picture-alliance/NurPhoto/W. Szymanowicz

May, ambaye aliingia  madarakani  katika  wadhifa  huo  wa  juu kabisa  katika  kipindi cha  mtafaruku ambacho  kilifuatia  kura  ya maoni  ya  mwaka 2016 kuhusiana  na  uanachama  wa  Umoja  wa Ulaya, ameshindwa  mara  kadhaa  kulifanya bunge  kuidhinisha makubaliano  yake  ya  kujitoa  kutoka  Umoja  wa  Ulaya  ambayo amepigia  upatu  kuwa  ni  njia  ya  kuponya  mgawanyiko  uliopo wa Brexit  nchini  humo.

Kura ya pili ya maoni

Lakini  katika juhudi  zake  za  mwisho, akitoa uwezekano wa  kuwa  na kura  ya  pili  ya  maoni  pamoja  na  utaratibu  wa  ukaribu  wa kibiashara na Umoja  wa  Ulaya , zimezusha  uasi kutoka  kwa baadhi  ya  mawaziri  wanaounga  mkono  Brexit. Kiongozi wa wabunge wa chama  cha  Conservative bungeni Andrea Leadsom amejiuzulu na huenda  wengine  zaidi wakafuatia.

Großbritannien | Andrea Leadsom, britische Ministerin für Parlamentsfragen tritt zurück
Andrea Leadsom waziri wa bunge la Uingereza aliyejiuzuluPicha: picture-alliance/dpa/NurPhoto/W. Szymanowicz

Alipoulizwa  kwanini  anajiuzulu  sasa Leadsom  alisema.

"Kwa sababu nimekuwa  nikiunga  mkono Brexit kwa jumla kwa miaka mitatu iliyopita na siwezi tena, kama  kiongozi wa  baraza la wawakilishi nikiwa  na  jukumu la kibunge, nikisimama katika maswali na  majibu kesho  na  kutangaza mswada  ambao  una  vipengee ambavyo  siwezi kuviunga mkono, ambavyo si  vya  Brexit."

Deutschland Treffen Theresa May mit Angela Merkel in Berlin
Muandamanaji ambaye anapinga Uingereza kujitoa Umoja wa UlayaPicha: DW/C. Albrecht

"Siamini  tena kwamba mtazamo wetu unaweza kufanikisha  matokeo ya  kura ya maoni," Leadsom , mmoja  kati ya  waliowania  kiti cha waziri  mkuu pamoja  na  May, alisema  katika  barua yake ya kujiuzulu.

May, ambaye  ameonesha ushupavu katika kipindi ambacho kimekuwa na hali ngumu ya vurumai akiwa waziri mkuu katika historia ya hivi  karibuni  nchini  Uingereza, ameahidi  kuondoka  madarakani iwapo wabunge wataidhinisha makubaliano yake  ya  Brexit lakini kwa sasa yuko  katika  shinikizo kubwa  kutaaj tarehe ya kuondoka.

Mwandishi: Sekione Kitojo / rtre

Mhariri: Josephat Charo