Unaweza kujiuliza kwanini upigaji picha za kuweka mitandaoni limekuwa jambo kubwa siku hizi? Mikahawa mingi imeanza kutumia fursa ya Instagram Food kuendana na kasi ya matumizi ya mitandao ya kijamii na hivi sasa inazingatia ubunifu zaidi wa picha za mitandaoni kama vile taa za rangi tofauti, mapambo ya kuvutia, mito, viti na meza.