1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Sarkozy ahukumiwa kifungo cha miaka mitatu

17 Mei 2023

Mahakama moja ya rufaa nchini Ufaransa leo imemhukumu kifungo cha miaka mitatu rais wa zamani wa nchi hiyo Nicolas Sarkozy, kwa ufisadi na ushawishi.

https://p.dw.com/p/4RUcD
Frankreich | Bestechungs-Prozess gegen Ex-Präsident Sarkozy
Picha: Bertrand Guay/AFP/dpa/picture alliance

Mahakama hiyo imesema anastahili kutumikia kifungo cha nyumbani cha mwaka mmoja akiwa amevalia bangili ya kielektroniki.

Sarkozy aidha amepigwa marufuku kushikilia wadhifa wowote wa umma kwa kipindi cha miaka mitatu kufuatia kitendo chake cha  kujaribu kumshawishi jaji katika kesi iliyokuwa inamkabili, ushawishi alioufanya ukiwa uligunduliwa kwa njia ya udukuzi.

Sarkozy, mwenye umri wa miaka 68 aliondoka mahakamani akiwa kimya ila wakili wake akasema watakata rufaa dhidi ya uamuzi huo katika mahakama ya juu zaidi ya rufaa nchini Ufaransa.

Tangu kuondoka madarakani, Sarkozy ambaye alikuwa kiongozi wa nchi hiyo kati ya mwaka 2007 hadi 2012, amekuwa akiandamwa na kesi.