Tume ya haki za binadamu Afrika imearifu juu ya ziara ya kutathimini hali ya uvunjifu wa haki za binadamu katika tarafa ya Loliondo na hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha Tanzania, ambapo pamoja na mambo mengine sehemu ya taarifa hiyo inasema kuwa baadhi ya wakazi wa Ngorongoro hawakushirikishwa katika zoezi la kuhamishwa na sasa wanakosa huduma muhimu. Zaidi alituarifu Veronica Natalis.