1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rais wa Somalia aongoza vikosi kupambana na al-Shabaab

Hawa Bihoga
19 Oktoba 2023

Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amewasili katika mji wa Baidoa ulio kusini magharibi mwa nchi hiyo kukusanya vikosi na kuanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya kundi la al-Shabab katika eneo hilo.

https://p.dw.com/p/4Xkt0
Somalia Präsident Hassan Sheikh Mohamud
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia.Picha: Farah Abdi Warsameh/AP/picture alliance

Taarifa ya ofisi ya rais huyo siku ya Jumatano (Oktoba 18) ilisema Mohamud anapanga kuanzisha awamu ya pili ya operesheni dhidi ya kundi hilo la wapiganaji katika majimbo ya kusini magharibi na eneo la Juba.

Mnamo Oktoba 7, kiongozi wa jimbo la kusini magharibi, Abdiaziz Hassan Mohamed, na maafisa wakuu wa usalama walifanya mkutano na kutangaza kuanza kwa operesheni dhidi ya al-Shabaab.

Soma zaidi:Kenya kuitangazia vita al-Shabaab 
Marekani yatowa dola $5M kumpata kiongozi wa al-Shabaab

Katika kipindi cha miezi michache iliyopita, rais wa Somalia alikuwa katika mikoa ya kati ambako bado serikali haijafanikiwa kurejesha udhibiti wa miji mikubwa kutoka kwa washirika hao wa kundi la al-Qaida, licha ya kuungwa mkono na wanamgambo wa koo katika mashambulizi hayo.