1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin: Mazungumzo yanawezekana, lakini bila Zelensky

29 Januari 2025

Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema nchi yake inaweza kufanya mazungumzo ya amani na Ukraine, lakini amefutilia mbali uwezekano wa kuzungumza moja kwa moja na Rais Volodymyr Zelensky, aliyemuita "asiyestahili".

https://p.dw.com/p/4pliQ
Rais Vladimir Putin wa Urusi
Rais Vladimir Putin wa Urusi.Picha: Mikhail Tereshchenko/TASS/dpa/picture alliance

"Unaweza kujadiliana na mtu yeyote, lakini kwa sababu yeye hana sifa, hana haki ya kusaini chochote. Lakini ikiwa anataka kushiriki kwenye mazungumzo, nitawatuma watu wanaofaa ambao watafanya mazungumzo haya." amesema Putin. 

Amesema kiongozi huyo wa Ukraine si halali kwa kuwa muda wake wa urais uliisha wakati kulipotangazwa sheria ya kijeshi.

Putin aidha, amedai kwamba mapigano huenda yakamalizika baada ya miezi miwili ama chini ya hapo, ikiwa mataifa ya magharibi yataacha kuisaidia Ukraine.

Kiongozi huyo wa Ukraine alijibu matamshi yao ya Putin akisema "anaogopa" mazungumzo na alikuwa akitumia "hila za kijinga" kurefusha mzozo wa karibu miaka mitatu.