1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMarekani

Putin kujibu mpango wa Marekani wa kupeleka silaha Ujerumani

28 Julai 2024

Urusi huenda ikaanza kutumia silaha mpya za mashambulizi kujibu mpango wa Marekani wa kupeleka makombora ya masafa marefu na ya kasi ya juu nchini Ujerumani. Haya yamesema leo na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

https://p.dw.com/p/4ipy9
Rais wa Urusi Vladimir Putin wakati wa hotuba yake ya kila mwaka kwa bunge la Urusi mnamo Februari 29,2024
Rais wa Urusi Vladimir PutinPicha: Evgenia Novozhenina/REUTERS

Akiongea wakati wa gwaride la wanamaji huko St Petersburg, Putin aliapa kuchukuwa hatua hiyo baada ya Marekani mapema mwezi huu kutangaza kuwa itaanza kupeleka silaha hizo Ujerumani katika mwaka 2026, ili kuthibitisha kujitolea kwake kwa jumuiya ya kujihami ya NATO na ulinzi wa Ulaya kufuatia uvamizi wa Urusi nchini Ukraine mnamo Februari 2022.

Soma pia: Mawaziri wa ulinzi wa Marekani na Urusi wajadiliana kupunguza hatari ya kusambaa mvutano

Putin amesema ikiwa Marekani itatekeleza mpango huo, Urusi itajichukulia kuwa huru kutoka kwa usitishaji wa awali wa pande moja wa kupelekwa kwa

silaha za mashambulizi za masafa ya kati na mafupi ikiwa ni pamoja na kuongeza uwezo wa vikosi vya pwani vya jeshi lake la wanamaji.