Mohammed Khelef anaongoza Maoni Mbele ya Meza ya Duara ambapo wachambuzi Abdulrahman Mohammed akiwa London, Mohamed Saleh akiwa Paris na Bravious Kyahoza akiwa Dar es Salaam wanajadili athari za kirusi cha corona kwenye uchumi wa dunia na hasa hatua ambazo mataifa ya Afrika Mashariki zinaweza kuzichukuwa kukabili hatari ya mserereko wa kiuchumi unaokhofiwa kutokana na ugonjwa wa COVID-19.