1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaGabon

Marekani yasitisha misaada isiyo ya kiutu nchini Gabon

27 Septemba 2023

Marekani imesitisha misaada mingi isiyo ya kiutu nchini Gabon baada ya utawala wa kijeshi kuchukua dhamana ya taifa hilo mwezi uliopita.

https://p.dw.com/p/4WqMP
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken ametangaza uamuzi wa Marekani wa kusitisha misaada nchini Gabon baada ya mapinduzi
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken ametangaza uamuzi wa Marekani wa kusitisha misaada nchini Gabon baada ya mapinduziPicha: Eduardo Munoz/REUTERS

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken ametangaza kusimamishwa kwa misaada hiyo ya kigeni nchini Gabon, na kusema wanafanyia mapitio ya mazingira yaliyochochea kuangushwa kwa aliyekuwa rais Ali Bongo Ondimba.

Blinken amesema kwenye taarifa kwamba hatua hiyo haitaathiri operesheni za serikali ya Marekani nchini Gabon, ingawa haikueleza zaidi ni shughuli zipi zinazofadhiliwa na Marekani zitakazoguswa na kiasi gani cha fedha kitasitishwa.

Gabon ni taifa la pili kufanya mapinduzi ya kijeshi baada ya Niger mapema mwaka huu. Marekani pia imesitisha baadhi ya misaada nchini Niger, ingawa bado haijabainisha rasmi kama kilichofanika ni mapinduzi.