1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mapigano makali yazuka kati ya jeshi la DRC na waasi wa M23

10 Februari 2023

Mapigano makali yalizuka tena Alhamisi kati ya jeshi la Jamuhuri ya kidemokakrasia ya Congo na waasi wa M23 katika vijiji vya Luhonga na Kingi.

https://p.dw.com/p/4NJxo
DR Kongo Ein M23-Rebellen
Picha: GLODY MURHABAZI/AFP via Getty Images

Mapigano hayo yalitokea kilometa 8 kaskazini mwa mji wa Sake mkoani Kivu ya kaskazini.

Maelfu ya raia walilazimika kukimbia huku baadhi wakielekea mji wa Goma na wengine katika mkoa jirani wa kivu kusini. 

Hali iliendelea kuwa ya wasiwasi mchana kutwa wa jana Alhamisi kwenye vijiji vya Kimoka na Luhonga vinavyoukaribia mji mdogo wa Sake ulioko umbali wa kilometa 27 magharibi mwa mji wa Goma, ambako maelfu ya raia walikimbia wakati jeshi la Congo lilikuwa likikabiliana na waasi wa M23.

Mkuu wa UNHCR ziarani Burundi kuwatembelea wahamiaji wa DRC

Wakizungumza na DW, raia hao baadhi ikiwa ni watoto na wanawake walilazimika kutembea kwa mguu kuelekea mjini Goma ambao umesalia mji pekee wa kukimbilia kwa maelfu ya raia wanaohangaishwa na vita hivyo.

Machafuko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamewalazimisha maelfu ya wakaazi kuyakimbia makwao.
Machafuko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamewalazimisha maelfu ya wakaazi kuyakimbia makwao. Picha: Nicholas Kajoba/Xinhua/IMAGO

Hadi Alhamisi jioni, wananchi wa Sake walionekana wakiwa wamepiga kambi kando na barabara wakiwa wamebeba mizigo na mifugo yao lakini bila matumaini ya kurudi tena majumbani kwao kutokana na milio ya risasi iliyoendelea kusikika kando na mji huo wa kimkakati wilayani masisi.

Mzozo wa Kongo wajadiliwa Bujumbura

Mapigano kati ya waasi wa M23 na jeshi la congo,yameendelea kushika kasi katika baadhi ya maeneo mkoani kivu kaskazini licha ya kuwepo kwa mikutano ya viongozi wa kikanda jijini luanda na Nairobi ,kulitaka kundi hilo kuondoka katika maeneo yote linalodhibiti.

Hata hivyo, wabunge wa eneo hili wamelaani  mapigano hayo huku wakilitaka jeshi kuwa na nidhanamu ambayo ni njia pekee ya kushindana na adui.

Papa Francis awataka Wakongo kusamehe

Mapigano hayo ya jana yanakuja baada ya waasi hao wa M23 kuuteka mji wa kimkakati wa kitshanga na kuongeza hofu kubwa kwa raia.