1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Makampuni mawili ya majani ya chai ya Kenya yafutiwa vibali

12 Mei 2023

Shirika moja la kimataifa limesema limeyafutia kibali cha idhini makampuni mawili makubwa ya kenya ya usafirishaji majani ya chai duniani baada ya kufanyika uchunguzi kuhusu unyanyasaji wa kingono

https://p.dw.com/p/4RHjP
Teeernte in Kenia
Picha: Billy Mutai/AA/picture alliance

Rain Forest Alliance ambalo ni moja ya mashirika makubwa ya kuidhinisha bidhaa za maendeleo endelevu duniani, limesema lilianzisha uchunguzi baada ya makala moja ya shirika la utangazaji la Uingereza BBC mwezi Februari kuangazia madai ya kusambaa kwa matukio ya unyanyasaji wa kingono katika mashamba ya majani ya chai. Uamuzi wa shirika hilo unamaanisha sasa  Kampuni ya James Finlay (Kenya) Ltd na ile ya ekaterra Tea Kenya Plc, haziwezi tena kuuza bidhaa zao kupitia kibali cha shirika hilo. Kenya ni moja ya wasafirishaji wakubwa wa bidhaa hiyo. Kampuni ya Rainforest Alliance imesema bado inaendelea kuahidi kutimiza wajibu wake kusaidia kukomesha unyanyasaji wa kingono pamoja na ukatili wa majumbani katika mtandao wa kusafirisha majani chai duniani.