Sudi Mnette amezungumza na Abigael Kiprono, mwanamzingira kutoka Kenya lakini pia ni miongoni mwa vijana walioratibu kongamano mbadala la kimataifa la mtandaoni la Mock Cop 26, wakijaribu kuziba nafasi ya mkutano wa kilele wa mabadiliko ya tabia nchi Cop 26 ambao kwa mwaka huu ulisitishwa kutokana na janga la virusi vya corona. Mkutano huo ulipangwa kufanyika Uingereza kuanzia Novemba 9 hadi 19.