1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kifo cha Nkurunziza: Viongozi watuma salamu za rambirambi

Amida ISSA, DW-BUJUMBURA10 Juni 2020

Viongozi wa taasisi mbalimbali Burundi na raia wa nchi hiyo wanaomboleza kifo cha Rais Pierre Nkurunziza. Salam za rambi rambi zimetolewa pia na wanabalozi wanao ziwakilisha nchi zao nchini humo.

https://p.dw.com/p/3dacq
Burundi Pierre Nkurunziza 2004
Picha: Getty Images/AFP/G. Guercia

Rais wa zamani Domitien Ndayizeye amesema licha ya kuwa bado ni mapema wanatambua kuwa kulingana na katiba

atakaye iongoza nchi kimpito ni spika wa bunge.

Kifo cha rais Pierre Nkurunziza kimezusha hali ya taharuki kwa raia wengi. Shughuli zimeonekana kudorora, 

huku redio na televisheni ya taifa ikibadili ratiba na kucheza nyimbo peke za dini za maombolezi.

Maafisa wakuu wa taasisi mbali mbali ikiwa ni pamoja na spika wa bunge, mkuu wa seneti, makamu

wa rais, Mawaziri wa serikali,  Msuluhishi wa kitaifa, baadhi ya wanasiasa, na hata raia wa kawaida wametowa
salaam za rambi rambi kwa familia yake rais Nkurunziza na chama chake Cndd Fdd.

Pia wanabalozi wa nchi za Kenya, Misri, Nigeria, Cote d, ivoire, Uturuki, China, na urusi tayari wamesaini kwenye kitabu cha maombole
kilozinduliwa kwenye ikulu ya rais.

Risala za maombolezi zimetolewa pia na marais wa zamani. Domitien Ndayizeye aliyefanya naye kazi Nkurunziza kama waziri wake wa dola anaye
husika na utawala bora,  amesema kuna umuhimu serikali kubaini kitakacho fuatia. Hata hivyo amesema katiba iko wazi ambapo atakaye
ongoza kimpito ni spika wa bunge.
Chama cha hayati Nkurunziza cha  Cndd Fdd bado hakijatoa taarifa yoyote, mbali na rais mteule Evariste Nsayishimiye aliyeshinda kwenye uchaguzi
ulofanyika Mei 20 kutowa salam za rambi rambi na kubainisha kuwa ataendelaza sera yake rais Nkurunziza.

Taarifa ya kifo cha rais Pierre Nkurunziza ilitangazwa na serikali hapo jana na kueleza  kuwa kifo chake kimesababishwa na
mshituko wa moyo.

Licha ya kazi kuendelea kufanyika, serikali ilitangaza  Msiba wa kitaifa wa siku 7 ambapo bendera zinapandishwa nusu mlingoti.
Rais Pierre Nkurunziza alifariki Jumatatu wiki hii baada ya kuiongoza Burundi kwa muda wa miaka 15.

Amida ISSA, DW -BUJUMBURA

Rais wa zamani wa Burundi Domitien Ndayizeye akimkumbatia Rais Nkurunziza alipoapishwa kwa mara ya kwanza kuwa rais mwaka 2005. (Picha ya maktaba)
Rais wa zamani wa Burundi Domitien Ndayizeye akimkumbatia Rais Nkurunziza alipoapishwa kwa mara ya kwanza kuwa rais mwaka 2005. (Picha ya maktaba)Picha: Getty Images/AFP/M. Longari