Mwanasiasa mashuhuri visiwani Zanzibar, Ismail Jussa, ambaye alishambuliwa baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020, amerejea rasmi kwenye uwanja wa siasa hali ambayo imezusha hamasa, hasa ikizingatiwa ukaribu wake na aliyekuwa makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar, Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad, aliyefariki dunia mwezi Februari mwaka huu. Sikiliza mahojiano kamili na Mohammed Khelef.