Janga jipya la wakimbizi kutoka jamii ya Waislamu ya Warohingya ambapo wengi wao wanaishi katika mkoa wa Rakhine nchini Myanmar lilianza Agosti 25, ambapo walilazimika kukimbia operesheni ya Jeshi la nchi hiyo. Katika Makala ya Mbiu ya Mnyonge tunaliangazia janga hili la jamii ya Rohingya nchini Myanmar. Ungana naye Mohammed Abdul-Rahman kwa mengi zaidi.