1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUjerumani

MOSCOW: Scholz yupo sahihi kutaka uchunguzi wa Nord Stream

9 Septemba 2024

Urusi imesema, Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz yupo sahihi kutaka uchunguzi wa kina ufanyike juu ya shambulio kwenye bomba la gesi la Nord Stream lililofanywa mwaka 2022.

https://p.dw.com/p/4kQi5
Hujuma kwenye bomba la Nord-Stream
Picha hii ilitolewa na Kamandi ya Ulinzi ya Denmark ikionyesha kuvuja kwa gesi katika bomba la Nord Stream 2 karibu na Bornholm.Picha: Danish Defence Command/dpa/picture alliance

Urusi imesema hayo, katikati ya kile ilichoita majaribio ya baadhi ya nchi za Magharibi kunyamazisha kile kilichotokea.

Scholz alisema katika mahojiano na televisheni ya Ujerumani mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba Ujerumani itahakikisha kuwa hakuna kitu kitakachofichwa katika uchunguzi huo na kwamba waliohusika na hujuma hiyo wataadhibiwa.

Urusi imelalamika mara kwa mara kwamba Ujerumani haijafanya vya kutosha kuchunguza hujuma hizo zilizosababisha mabomba mawili ya Nord Stream kupasuka. Mabomba hayo yalijengwa kusafirisha gesi ya Urusi hadi Ulaya chini ya Bahari ya Baltic.

Mwezi uliopita waendesha mashtaka wa Ujerumani walitoa hati ya kuwezesha kukamatwa kwa mkufunzi wa kupiga mbizi wa Ukraine nchini Poland kuhusiana na mashambulizi hayo.