GAZA:Wapalestina wauwawa Gaza
28 Aprili 2007Matangazo
Wanajeshi wa Israel wamewauwa wapalestina watatu na kumjeruhi mmoja katika ukanda wa Gaza.
Duru za Palestina zinaarifu mashambulio ya risasi yamefanyika mapema hii leo asubuhi kaskazinimagharibi mwa mji wa Gaza na karibu na eneo la usalama.
Mwanajeshi wa Israel amethibitisha shambulio hilo na kusema wapalaestina hao walikuwa wakijaribu kuweka mabomu katika eneo hilo kati ya Gaza na Israel.