CHADEMA yatangaza kutosusia uchaguzi mkuu wa Tanzania
12 Februari 2025Matangazo
Akihutubia taifa leo amesema, CHADEMA kitaishtaki serikali ya Tanzania kwa wananchi, jumuiya za kimataifa na viongozi wa kidini ili kuhamasisha mabadiliko ya katiba na sheria za uchaguzi zinazochagiza mifumo mibaya ya uchaguzi inayovunja demokrasia.
Lissu aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama hicho Januari 22 amesema mifumo ya uchaguzi Tanzania inadhibitiwa na Rais wa nchi na kwa upande wa Zanzibar pia ukidhibitiwa na Rais.
Soma pia:Chadema yakamilisha hatua ya kwanza ya uchaguzi wa mabaraza
Amesema mfumo huo wa uchaguzi wa Tanzania ulisababisha Tanzania kuongozwa na viongozi ambao hawakupigiwa kura kati ya mwaka 2019/2020.