1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bunge laridhia kuchelewesha Brexit

15 Machi 2019

Baada ya Uingereza kupiga kura jana usiku kuomba mchakato wa kujiondoa kutoka kwenye Umoja wa Ulaya unaojulikana kama Brexit kurefushwa kwa miezi mitatu mbele, kumekuwa na maoni mbalimbali baada ya kura hiyo

https://p.dw.com/p/3F72h
UK Unterhaus lehnt zweites Brexit-Referendum ab
Picha: Reuters TV

Bunge la Uingereza limepiga kura kukubali kuongezewa muda wa kujiondoa kwa nchi hiyo kutoka kwenye Umoja wa Ulaya kwa kura 412 zilizokubali dhidi ya kura 202 zilizotaaa. Kabla ya hapo Uingereza ilipaswa kuondoka kisheria kutoka Umoja wa Ulaya Machi 29.

Lakini sababu bunge hilo lilikataa mpango wa Waziri Mkuu Theresa May siku ya Jumanne, ilibidi waombe kuongeza muda wa mchakato huo.

Kuongezwa huko muda inabidi pia kukubaliwa na nchi 27 za Umoja wa Ulaya katika mkutano wao wa kilele Machi 21 na 22. 

Wahafidhina na uwezekano wa Brexit ya mapema

Anayeonekana kuwa makamu wa Waziri Mkuu wa Uingereza, David Lidington, ameliambia shirika la habari la Uingereza, BBC kwamba bado nchi hiyo inataka kujiondoa kutoka kwenye Umoja wa Ulaya kwa kufata utaratibu maalum na bado ina mpango wa kutoka Machi 29, labda kama kutakuwa na mpango mbadala.

Lidington aliongeza kusema kuwa, ana matumaini bado wanaweza kutoka kwenye Umoja wa Ulaya hivi karibuni kwa kufuata utaratibu, lakini hiyo inategea kama bunge litayapitisha hayo makubaliano ya kujitoa na kutekeleza sheria zitakazofuata kabla ya na kupitisha mkataba huo wa kujitoa.

Amesema mpaka mwisho wa Machi, inabidi kuwe na mbadala, sio tu maazimio ya bunge, bali wanapaswa kuwa na mapendekezo pamoja na utatuzi ambao utawezesha kuwa na urefushwaji bila ya mgongano siku ya Machi 29.

Labour wataka kura ya pili ya maoni

UK Unterhaus für Brexit-Verschiebung und drittes Votum über Abkommen | Jeremy Corbyn
Jeremy Corbyn mbunge wa chama cha upinzani cha LabourPicha: Reuters TV

Kwa upande mwingine, kiongozi wa chama cha Labour, Jeremy Corbin, amesema Theresa May inabidi akubali kwamba mpango wake wa kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya hauwezekani tena na pia kujiondoa kutoka umoja huo bila makubaliano pia haiwezekani.

Hivyo Corbin anaunga mkono kura ya pili ya maoni kwa Uingereza kujitoa kwenye Umoja wa Ulaya kama njia mbadala ya kuondoka katika mgogoro wa Brexit.

Aliyazungumza hayo baada ya bunge la Uingereza kupiga kura ya kuongeza muda wa kujiondoa, ingawa bunge hilo limekataa kura ya pili ya maoni kuhusu Brexit.

Mwandishi: Harrison Mwilima/RTRE1/ APE

Mhariri: Grace Patricia Kabogo