1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Belarus yatuma wanajeshi wake mpakani na Ukraine

10 Agosti 2024

Belarus imetuma wanajeshi wake katika eneo la mpakani kuimarisha usalama katika eneo hilo, ikisema kuwa droni za Ukraine zimekiuka anga yake wakati wa operesheni ya Kiev katika eneo la Urusi la Kursk.

https://p.dw.com/p/4jKVl
Lukashenko
Rais wa Belarus Alexander Lukashenko Picha: Alexander Zemlianichenko/AP/picture alliance

Rais Alexander Lukashenko amesema mifumo ya ulinzi wa anga, imeharibu droni hizo za Ukraine baada ya kuingia katika anga ya taifa hilo katika eneo la Mashariki la Mogilev linalopakana na Urusi. 

Lukashenko ameongeza kuwa droni nyengine ziliharibiwa karibu na mji wa Urusi wa Yaroslavl. Waziri wa ulinzi wa Belarus Viktor Khrenin, amesema kufuatia hali inayoshuhudiwa nchini Ukraine na Kursk, kamanda mkuu wa jeshi ameamuru wanajeshi kupelekwa katika maeneo ya kimkakati ya Gomel na Mozyr ili kujibu uchokozi wa aina yoyote.  

Urusi yajibu mashambulizi ya Ukraine kwa kuanzisha operesheni ya kijeshi

Amesema wanajeshi wa operesheni maalum, wanajeshi wa ardhini na mifumo kadhaa ya kuzuwia makombora yamewekwa tayari kujibu mashambulizi ya aina yoyote dhidi ya taifa lake. Amesema ukiukwaji wa anga yake ni uchokozi na wako tayari kujibu.