1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Baerbock kuhudhuria ufunguzi wa kiwanda cha chanjo Rwanda

17 Desemba 2023

Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Annalena Baerbock anakwenda Rwanda kuhudhuria Ufunguzi wa kiwanda cha kwanza barani Afrika cha kutengeneza chanjo ya (mRNA) ya Uviko-19.

https://p.dw.com/p/4aGkA
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Annalena Baerbock
Waziri wa mambo ya kigeni wa Ujerumani Annalena BaerbockPicha: Sebastian Rau/photothek/picture alliance

Kwa mujibu wa wizara ya maendeleo ya Ujerumani, serikali mjini Berlin inaunga mkono inaunga mkono juhudi za utengenezaji endelevu wa chanjo hiyo barani Afrika kulisaidia kujiandaa kwa ajili ya kukabiliana na miripuko ya siku za baadae.

Kampuni ya utengenezaji dawa ya BioNtech yenye makao yake mjini Mainz inapanga kutengeneza chanjo hiyo kwa teknolojia ya mRNA katika kiwanda hicho cha Kigali kuanzia mwaka Ujao.

Kuna uwezekano pia wa chanjo nyingine kama hizo dhidi ya Malaria na kifua Kikuuu  kutengezwa katika kiwanda hicho katika miaka ya baadae endapo kibali cha kuidhinisha hatua hiyo kitatolewa.

Ujerumani inachangia  zaidi ya Yuro Milioni 550 katika kuusaidia Umoja wa Afrika kufikia lengo lake la kutengeneza asilimia 60 ya chanjo zinazotumika barani humo kufikia mwaka 2040.

Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Annalena Baerbock anatarajiwa kukutana na mwenzake wa Rwanda Vincent Biruta mjini Kigali na kutembelea makumbusho ya wahanga wa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.