Kila kukicha vijana wanazidi kuibuka na ubunifu katika sekta tofauti kwa kutumia teknolojia. Sauti Kitabu ni Programu mpya ambayo imeanzishwa, ikiwa ni jukwaa la simulizi za sauti kwa lugha ya Kiswahili. Programu hiyo imeanzishwa kwa ushirikiano wa vijana wawili kutoka Tanzania na Finland. Sikiliza makala hii ya Sema Uvume kuijua kwa undani.