1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Annan ahimiza uchaguzi wa amani Kenya

Josephat Nyiro Charo25 Februari 2013

Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, ameonya leo kwamba vitisho, uhasama wa kikabila na machafuko, huenda vikauhujumu uchaguzi mkuu wa Kenya unaotarajiwa kufanyika Machi 4.

https://p.dw.com/p/17kiP
Kofi Annan, joint special envoy for the United Nations and the Arab League, gestures during a news conference at Sheremetyevo International Airport outside Moscow, March 26, 2012. Annan said on Monday that the crisis in Syria "cannot drag on indefinitely" but that he could not set a deadline for a resolution after a year of bloodshed. REUTERS/Denis Sinyakov (RUSSIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Kofi AnnanPicha: Reuters

Annan, ambaye alisaidia kuikoa Kenya isitumbukie katika machafuko makubwa miaka mitano iliyopita, amesema nchi hiyo iko katika mkondo sahihi kufuatia machafuko ya baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 yaliyosababisha vifo vya watu zaidi ya 1,000 na kuwalazimu wengine takriban 600,000 kuyakimbia makazi yao. Amewakumbusha Wakenya kwamba nchi yao imesimama katika poromoko la kujiangamiza yenyewe, kuzingatia vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi uliopita.

"Chaguzi lazima zifanyike kwa amani, uhuru na haki. Lazima zifanywe kwa mujibu wa sheria, kwa uadilifu na zionyeshe ari ya wananchi. Hapo ndipo umoja wa kitaifa, uthabiti na utangamano vitakapolindwa," amesema Annan katika taarifa yake.

"Matukio ya hivi karibuni ya machafuko na ongezeko la hali ya wasiwasi kuelekea uchaguzi, vinatia wasiwasi mkubwa sana. Kenya haiwezi kuhatarisha kurejea tena katika siku mbaya za huzuni, masikitiko na giza," akaongeza kusema Kofi Annan.

Kenyan President Mwai Kibaki, left, and former U.N. Secretary-General Kofi Annan, center, and opposition leader Raila Odinga, right, observe a minute of silence for the victims of the recent violence, Tuesday, Jan. 29, 2008 during the opening of the "dialogue process," in Nairobi. Kibaki and Odinga together with mediator Annan formally opened the "dialogue process," with the rivals under international pressure to share power. Odinga insisted what needed "the most urgent attention" was the resolution of the flawed election results, an issue Kibaki has indicated is not negotiable.(AP Photo/Karel Prinsloo)***Zu Dohrenbusch, Keine Entspannung der Lage in Sicht - Kenianischer Oppositionspolitiker in Nairobi erschossen***
Kofi Annan (katikati) Mwai Kibaki na Raila OdingaPicha: AP

Annan amesaidia mchakato wa amani

Mapema mwaka 2008, Annan alisaidia kufikiwa muafaka wa kisiasa kati ya wagombea wawili wakubwa wa urais wakati huo. Makubaliano hayo yalimuwezesha Mwai Kibaki kubakia kuwa rais na mpinzani wake mkuu, Raila Odinga, akawa waziri mkuu. Kibaki hagombei wadhifa wowote katika uchaguzi ujao, kwa kuwa kisheria amekamilisha muda wake kama rais wa nchi, lakini Odinga ni miongoni mwa waombea wanane wanaowania kuingia ikulu.

Katika taarifa yake, Annan amewaasa Wakenya kuwa uchaguzi hautakiwi kuangaliwa kama shindano ambapo mshindi atachukua kila kitu. Amekumbusha kwamba Kenya ina katiba mpya na idara ya mahakama iliyoimarika. Ametaka matokeo ya uchaguzi huru na wa haki yaheshimiwe na mivutano yote itakayojitokeza, isuluhishwe mahakamani.

Annan amekuwa akizuru mara kwa mara nchini Kenya kukutana na maafisa wa ngazi za juu, akiwa na matumaini ya kusaidia kuepusha machafuko ya uchaguzi. Lakini katibu huyo mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa hajaitembelea Kenya kwa miezi kadhaa kwa sababu baadhi ya viongozi wa nchi hiyo waliziona ziara zake kama hatua ya kuyaingilia masuala ya ndani ya taifa hilo.

U.S. Senator John Kerry (D-MA) testifies during his Senate Foreign Relations Committee confirmation hearing to be secretary of state, on Capitol Hill in Washington, in this January 24, 2013 file photo. Kerry on January 29, 2013 won the unanimous support of the Senate Foreign Relations Committee on Tuesday to replace Hillary Clinton as President Barack Obama's new secretary of state. REUTERS/Jonathan Ernst/Files (UNITED STATES - Tags: POLITICS HEADSHOT)
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani, John KerryPicha: Reuters

Kerry ataka uchaguzi usio na vurugu

Wakati huo huo, waziri wa mashauri ya kigeni wa Marekani, John Kerry, ametaka uchaguzi wa Kenya ufanyike kwa amani. Kerry amewahimiza Wakenya kufanya uchaguzi huru na wa haki bila kufanya machafuko. Ujumbe wake umewasilishwa kwa Wakenya wakati alipompigia simu rais wa Kenya, Mwai Kibaki.

"Nimezungumza na rais Kibaki. Sasa ni wakati wa Kenya kuungana pamoja, uchaguzi huru, wa haki na halali usio na machafuko – JK," wizara ya mambo ya kigeni imeandika katika mtandao wa kijamii wa Twitter.

John Kerry ndiye afisa wa hivi karibuni wa cheo cha juu wa Marekani kuzungumzia uchaguzi wa Kenya, ambao umepangwa kufanyika Machi 4, 2013.

Mwandishi: Josephat Charo/APE
Mhariri: Bruce Amani