1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AKK akabiliwa na mbinyo katika mkutano mkuu wa chama cha CDU

Sekione Kitojo
22 Novemba 2019

Baada  ya  kuwapo madarakani  kama  mwenyekiti  wa  chama  cha CDU nchini  Ujerumani Annagret Kramp-Karrenbauer bado yuko  mbali na  lengo  lake , la  kuwa mgombea wa  kansela  kutoka  chama  hicho cha  kihafidhina.

https://p.dw.com/p/3TWBx
CDU-Bundesparteitag in Leipzig Gottesdienst
Picha: picture-alliance/dpa/H. Schmidt

 Uchunguzi wa  maoni  ya  wapiga  kura  unaonesha hali mbaya  kwake. Katika  mkutano  mkuu  wa  chama  mjini  Leipzig kwa hiyo  anapaswa  kuonesha  hali  tofauti  ili  kuwavutia wajumbe. 

CDU-Bundesparteitag in Leipzig
Matayarisho ya mkutano wa chama cha CDU mjini LeipzigPicha: picture-alliance/dpa/K. Nietfeld

Alikuwa  na  mpango  mkubwa , wa  kukiokoa  chama  hicho  cha  CDU kutoka  katika  mivutano  ya ndani, kukijenga  upya  na  kujihakikishia nafasi  ya  mbele  katika  mbio  za  kuelekea  kuwa  kansela. Annehret Kram - Karrenbauer, ambaye  pia  anafahamika  kama AKK, anabeba mfumo  wake binafsi. Ametembelea  matawi  mashinani  katika  chama hicho, akizunguka  nchi  nzima, akijaribu  kujiondoa  kutoka  katika taswira ya   Angela  Merkel, ambayo  asingependa  kuanza  akiwa kama  sehemu  ya  utawala  wake. Badala  yake  anataka kujitengenezea tawira  yake  akiwa  kiongozi  wa  chama  cha  CDU.

Lakini  muda  mfupi tu baadaye kila  kitu  kikawa  wazi , mpango  wake haukuweza  kusonga  mbele. Kama  mkuu  wa  chama  alikuwa anaonekana  bila  shaka  mgombea  wa  moja  kwa  moja  wa   wadhifa wa  kansela kupitia  chama  hicho, lakini maoni  ya  wapiga  kura  kwa upande  wake  yalipungua  hadi  nusu. Katika  wanasiasa  muhimu kumi  wa  Ujerumani, AKK  ameshika  nafasi ya  mwisho. Kwa  hiyo shaka  imekuwa  kubwa , iwapo  inawezekana  akateuliwa  kuwa mgombea  wa  wadhifa  wa  kansela.

Alijikwaa  mapema  katika  wadhifa  wa mwenyekiti  wa  chama  kwa kutoa  kichekesho ambacho  hakikupendeza  kuhusu  watu wanaofanya mapenzi  ya  jinsia  moja na  kuharibu  njia  yake  ya  kuingia  katika masuala  ya  dunia. Hadi  wakati  huo, kiongozi  huyo  mwenye  umri  wa miaka  57 alikuwa  katika  hali  nzuri  tu katika  chama  hicho ambacho viongozi  wake  wengi ni  wanaume. AKK  alijiunga  na  chama  cha CDU mwaka  1981 akiwa  mwanafunzi  bado.

CDU Motto Die Mitte Annegret Kramp-Karrenbauer
Annegret Kramp-Karrenbauer mwenyekiti wa chama cha CDUPicha: picture-alliance/dpa/K. Nietfeld

Ahamia  Berlin

Baada  ya  kuingia  rasmi  katika  masuala  ya  kisiasa  miaka  chini  ya 20  iliyopita katika  siasa za  majimboni, alihamia  mwezi  Februari mwaka  jana  katika  patashika ya  siasa  za  taifa mjini  Berlin  akiwa kama  katibu  mkuu  wa  chama  cha  CDU. Hii  ilikuwa  baada  ya kukiongoza  chama  katika  mafanikio  mara  mbili  ya  ushindi  wa uchaguzi  katika  jimbo  anakotoka  la  Saarland.

Akiwa  waziri wa  mambo  ya  ndani  na  waziri  mkuu  wa  jimbo  hilo alifanya  kazi  nzuri  sana, hadi  Angela  Merkel  akaamua  kumfuta kuja katika  mji  mkuu. Kazi nzuri  aliyoionesha AKK  katika  jimbo  lake alipaswa  pia  kuionesha  mjini  Berlin.  Mtaalamu  wa  masuala  ya kisiasa  mjini Bonn Frank Decker anatoa tathmini  yake  kuhusu  wadhifa wa  kansela.

"Ameshindwa kuonesha  kazi  nzuri  kama  mwenyekiti wa  chama, ambapo  chama kinapaswa  kumuunga  mkono na  kuwanyamazisha wakosoaji  wake. Anayetaka  kuingia  katika  mbio  za  kukiongoza chama , ni  lazima aoneshe uwezo  wake, ili aweze  kuchukua  pia wadhifa wa  kansela."

Berlin | Deutsch-Amerikanische Konferenz - Friedrich Merz und Annegret Kramp-Karrenbauer
Friedrich Merz (kushoto) akiwa pamoja na mwenyekiti wa chama cha CDU Annegret Kramp-KarrenbauerPicha: picture-alliance/dpa/W. Kumm

Alianza kama mtu wa  mbele kwa  Angela  Merkel, lakini Kramp-Karrenbauer  amekuwa  haraka  akifanya  makosa  mengi. Licha  ya kuwa  anafahamika  kuwa  mzungumzaji  mzuri, kuwa  kiongozi  wa chama  amekuwa hoi  mno kwa  upande  wa  uchaguzi.Akiwa  kama mkuu  wa  chama bila  ya  wadhifa  wa  waziri  Kramp-Karrenbauer hana  uzito  ndani  ama  nje  ya  nchi.

Iwapo hali ya maoni ya wapiga  kura  itaendelea  kubakia  mbaya  kama ilivyo, katika  chama  cha  CDU, kuna  hatari ya  kutokea  mivutano ndani  ya  chama. Ndio sababu  ni lazima  suala  hilo  lipatiwe ufumbuzi, katika  miezi  michache  ijayo. Friedrich Merz mmoja  wa  watu wanaowania  nafasi  ya  ukansela  baada  ya  kuelezea kuwa serikali imeoza , amerejea  nyuma  kidogo  na  kueleza  kuwa  asingependa kufanya  uasi  katika  serikali.

 

 LINK: http://www.dw.com/a-51346677