Bunge la Kenya limepitisha marekebisho tata ya sheria za uchaguzi kwamba mgombea mmoja akijiondoa kwenye kinyang’anyiro yule mwingine atakuwa mshindi na kuapishwa// Baraza la mawaziri la Uhispania linakutana leo kujadili njia za kujibu hatua ya kiongozi wa jimbo la Catalonia lenye mamlaka ya ndani, ambaye jana jioni alisema atasonga mbele katika azma ya kutangaza uhuru kamili wa jimbo hilo.