1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Blinken, Stoltenberg waonya mafanikio ya Ukraine

Bruce Amani
30 Januari 2024

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken ameonya kuwa mafanikio yaliyopatikana Ukraine katika kipindi cha miaka miwili ya mapigano yatatiliwa shaka kama hakutakuwa na ufadhili mpya wa Marekani.

https://p.dw.com/p/4bonv
Washington, Marekani | Antony Blinken na Jens Stoltenberg
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Jens Stoltenberg Picha: Alex Wong/AFP/Getty Images

Akizungumza katika kikao cha pamoja cha waandishi wa habari na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Jens Stoltenberg mjini Washington, Blinken amesema kuwa bila kutolewa fedha hizo za nyongeza, Marekani itakuwa inatuma ujumbe mzito na usio sahihi kwa maadui wake wote kuwa haiko makini kuhusu kuutetea uhuru, na kuitetea demokrasia.

Biden ameliomba bunge la Congress kuidhinisha dola bilioni 61 kama msaada mpya kwa Ukraine. Stoltenberg atakutana leo na wabunge ili kueleza jinsi hali ilivyo Ukraine.

Soma pia:Ukraine yataka uchunguzi wa kimataifa katika ajali ya ndege ya Urusi

Wabunge wa Republican wanasita kuendelea kuifadhili Kyiv, wakisema haina mkakati wa wazi wakati mapigano dhidi ya wanajeshi wa Rais wa Urusi Vladmir Putin yakiendelea.

Stoltenberg amesema kama Putin atashinda vita, itakuwa ni janga sio tu kwa Ukraine bali pia itafanya ulimwengu kuwa hatari zaidi na kila mmoja kukosa usalama.