Tangu mlipuko wa janga la Covid-19, kubisha, juhudi mbali mbali zimekuwa zikitekelezwa na serikali za mataifa za kukabiliana na kuenea kwa virusi vya Corona vinavyosambaa kwa kasi ya ajabu ulimwenguni. Hata hivyo, katikati ya wingu lenye kiza kinachotishia uhai wa binadamu, juhudi za kikundi kimoja cha vijana wahandisi nchini Kenya huenda zikaleta ahueni sio tu nchini humo lakini ulimwenguni.