1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Narges Mohammadi aishutumu serikali ya Iran kwa "ukidikteta"

10 Desemba 2023

Mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel aliyeko gerezani nchini Iran Narges Mohammadi, ameishutumu serikali ya Iran kwa udikteta na ukandamizaji wa wanawake.

https://p.dw.com/p/4ZzWJ
Norway, Tuzo ya amani ya Nobeli 2023
Watoto wa Mwanaharakati Narges Mohammadi wakipokea tuzo kwa niaba ya mama yaoPicha: Javad Parsa/NTB/picture alliance

Mohammadi ametoa shutuma hizo katika hotuba iliyotolewa na watoto wake mjini Oslo walipokuwa wanapokea tuzo hiyo kwa niaba yake.

Soma zaidi: Mshindi tuzo ya amani ya Nobeli kuanza mgomo wa kula gerezani

Watoto wake mapacha waliyo na miaka 17 Ali na Kiana, wanaoishi uhamishoni Ufaransa tangu mwaka 2015 walisoma hotuba hiyo iliyopenyezwa kutoka korokoroni iliyosisitiza kuwa watu wa Iran watafanikiwa kuondoa vizuizi na dhuluma dhidi yao. 

Narges anayepinga uvaaji wa hijabu wa lazima katika Jamhuri hiyo ya kiislamu na hukumu ya kifo inayotolewa huko amekuwa gerezani tangu mwaka 2021 na hakuweza kupokea tuzo yake.