Huku makali ya njaa yakiendelea kukithiri nchini Kenya, viongozi mbali mbali wamejitokeza kumhimiza Rais, Uhuru Kenyatta, kuutangaza ukame unaoshuhudiwa kuwa janga la kitaifa. Zaidi ya watu milioni mbili wanakabiliwa na kitisho cha kufa njaa huku jamii za wafugaji wa kuhamamahama zikipoteza mamia ya mifugo kila siku kutokana na ukame huo.