1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hali kinu cha nyuklia cha Kursk bado mbaya - Grossi

24 Septemba 2024

Mkuu wa Shirika la Kudhibiti Nguvu za Atomiki la Umoja wa Mataifa, Rafael Grossi, amesema hali bado ni mbaya kwenye kinu cha nyuklia cha Kursk nchini Urusi.

https://p.dw.com/p/4kzyl
Kursk | Rafael Grossi
Mkuu wa Shirika la Atomiki la Umoja wa Mataifa, Rafael Grossi (kushoto), akiwa na timu yake kukagua kinu cha nyuklia cha Kursk mnamo Agosti, 27, 2024.Picha: Rosatom/Handout via REUTERS

Kwenye mahojiano yaliyochapishwa leo na shirika la habari la Urusi, RIA,  Grossi amesema hali hiyo mbaya inatokana na kuwepo kwa harakati za kijeshi karibu na kinu hicho.  

Hata hivyo, mkurugenzi huyo ya shirika la atomiki la Umoja wa Mataifa amesema shirika lake halina mpango wa kuweka kikosi cha kudumu kwenye kinu hicho kama ambavyo limeweka kwenye vinu vyengine vinne nchini Ukraine, kikiwemo cha  Zaporizhzhia kilichochukuliwa na jeshi la Urusi mwanzoni kabisa mwa uvamizi wake Februari 2022.

Soma zaidi: Urusi inasema raia 56 waliuawa wakati Ukraine ilipolishambulia eneo la Kursk

Vikosi vya jeshi la Ukraine bado vipo kwenye mkoa wa kusini mwa Urusi, Kursk, baada ya uvamizi wao wa mwezi uliopita, lakini vimeweka kambi umbali wa kilomita 40 kutoka kwenye kinu hicho cha nyuklia.