Kulingana na mashirika ya kutoa misaada Afrika mashariki, takriban watu milioni 20 wanakabiliwa na njaa. Japo Kenya inayo nguvu kubwa kiuchumi katika kanda hiyo, pia inakumbwa na athari za ukame. Mzozo huo umekuwa mbaya zaidi kufuatia siasa ya ufisadi na misururu ya sera ambazo zimefeli.